Laiti Ningejua

Ilianza ka’ mzaha, imegeuka karaha
Donda latoka usaha, kaiba yangu furaha
Nilibugia tufaha, meiponza yangu raha
Laiti ningejua!
Blogu ya Mashairi
Ilianza ka’ mzaha, imegeuka karaha
Donda latoka usaha, kaiba yangu furaha
Nilibugia tufaha, meiponza yangu raha
Laiti ningejua!
Malkia nimemaka, vimbimbi vinanitoka
Binadamu megeuka, uongo unawatoka
Wadai mekengeuka, moto mkali wawaka!
Umekuwa ja sungura, zabibu kuzikwangua
Mashavu yamekufura, ya kwangu meyatua
Mbona hujui majira, ya kutangaa na jua?
Kila mchimba kisima, huingiya mwenyewee
Nakubali nimekosa, kuvunda wako mtima
Pembeni nilikutosa, yakuchukiza kasema
Kukataa yako posa, mrututu nikatema
Unisamehe swahibu, kisasi hakifaidi
Sumu hino sumu, yakereza ini
Sumu chungu sumu, nimo taabani
Sumu liza sumu, binti nifanyeni?
Usafi jambo muhimu, maanani tuliweke
Moyo tusitie sumu, fundo la inda siweke
Sithubutu kuhukumu, mola takupiga teke
Mtima wanituama, nafsi yanisukuma
Nasakamwa natema, yote mema tayasema
Maadili kitu chema , tayatetea daima.
Huno ndio udhalimu, kuuharibu uke
Wakeketaji ni sumu, wawaponza wanawake
Mola atawahukumu, kukosoa kazi yake
Ukatapo kinembe, haki wazikiuka!
Unaweza kupata App yetu mpya kutoka kwa Google Play Store na uweze kulisoma shairi hili vizuri kwa simu yako au kulihifadhi usome baadaye bila mtandao