Mapenzi ni Sumu

Penzi halina mwalimu, japo linayo mazao,
Wengi husema li tamu, sijaona ufaao,
Naeleza kwa nudhumu, lisomwe kila uchao,
Mapenzi kweli ni sumu, hudhuru wapendanao!
Blogu ya Mashairi
Mtiririko ni shairi ambalo vina vyake vya mwisho na vya kati havibadiliki kutoka ubeti wa kwanza hadi wa mwisho.
Penzi halina mwalimu, japo linayo mazao,
Wengi husema li tamu, sijaona ufaao,
Naeleza kwa nudhumu, lisomwe kila uchao,
Mapenzi kweli ni sumu, hudhuru wapendanao!
Nawaomba wasanifu, wajuzi wa hii kunga
Nifunzeni ubunifu, nami niitwe malenga
Nipange beti kwa safu, niwache kuunga unga
Wajuzi wa hii kunga, nifunzeni ubunifu.
Nawaomba wasanifu, wajuzi wa hii kunga,
Nifunzeni ubunifu, nami niitwe malenga,
Nipange beti kwa safu, niwache kuunga unga,
Wajuzi wa hii kunga, nifunzeni ubunifu.
Naomba niseme wazi, kwetu na liwe bayana,
Mja nataka maizi, unielewe kwa kina,
Ili tusiwe wajuzi, na Mola tukakosana,
Kupata sio idili, ni kudura za Rabana.
Kuna vingi duniani, vyenye tunu na thamani,
Vyavutia si utani, rahisi kuvitamani,
Ila kwangu vyote duni, pasi amani moyoni,
Taacha vyote lakini, nikachague amani.
Leo mwenyewe natubu, imeshanishinda fani,
Aula nitoe gubu, li’lo mwangu fuadini,
Msambe nawajaribu, nalonga pasi utani,
Miye nyumba ya udongo, vishindo vyazidi kani.
Lo! Pati wa patipati, atafutacho sipati
Pembeni hapitipiti, ila pote katikati
Avimeza vichapati, akiketi kaimati
Patii wa patipati, mbona nyumbani haketi?
Naipiga parapanda, watu wote sikieni,
Niwatoe njia panda, mnijue kiundani,
Hakuna ninachopenda, kama milima jamani,
Tambarare chukueni, milima niachieni.
Unaweza kupata App yetu mpya kutoka kwa Google Play Store na uweze kulisoma shairi hili vizuri kwa simu yako au kulihifadhi usome baadaye bila mtandao